Naomba Kuongea na Wadogo Zangu wa Kiume 18-30 Years...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Utu uzima dawa! Mnakopita sasa sisi tulishapita salama, lakini kuna uhitaji wa kukumbushana machache, kupeana mbinu na kutiana moyo pia (hapa kwa sehemu hata wadogo zangu wa kike watahusika). Naongelea mabadiliko ya makuzi kihomoni, kimtazamo, kimahusiano na kifikra pia. 

Niwapongeze pia wengi wenu kwa kuwa wawazi kwa yale mnayopitia, wengi wenu hamfahamu kuwa ni sehemu ya makuzi hivyo kujaa hofu na woga mwingi hasa kwenye maeneo haya;

1. Haiba - hapa kila mmoja anajitahidi awezavyo ili aonekane wa kisasa kwa mavazi lugha na hata mikogo mingineyo, kukosa baadhi ya hivyo vitu husababisha maumivu makubwa sana bila kutambua kuwa wakati wako wa kupata bado

2. Ukakamavu/confidence ya kuongea na hadhira au jinsia tofauti, hapa ni kimbembe, wengi hujichukia na kujistukia na hivyo kusababisha kujitenga na jamii muda mwingi kwa kudhani wengine wanajiona bora au ni mahiri kuliko wao! Hiki ni kipindi tu na kitapita lakini siri ya kuongea na hadhira ni kutowaangalia watu machoni bali kuwaangalia juu ya macho yao kwenye paji la uso.

3. Mahusiano kipengele hiki ni muhimu sana na hapa namaanisha kwenye ishu nzima ya kufanya mapenzi. Asikudanganye mtu, mapenzi utayajua baada ya kuvuka miaka 30, hapo utakuwa umewazoea na kuwafahamu wanawake na utakuwa huna hofu tena. wengi sana hapa wanalalamika kukosa nguvu au kumaliza haraka hii yote inaletwa na hofu na mara nyingi kudate mpenzi ambaye tayari keshakutana na wataalam, usitegemee kamwe katika miaka yako 26 umridhishe mwanamke wa 18-23 atakuwa anakuibia tuu. 

Mabinti wengi below 25 wapenzi wao ni 35+years. Hapo huwezi weka ligi.
Kinachowatisha wengi ni story za wanawake kufikishwa kileleni au kupiga show 30 nonstop wakati wewe dak5 nyingi. Usihofu, muda wako bado, wewe bado mchanga hujakomaa.

Lakini vile vile kuna wakati maungo yako huhitaji mapumziko. Hii hutokea yenyewe automatically, ndio maana kuna wakati unakuwa na ashiki sana na kuna wakati unakuwa kama hanithi. Usitishike, jitahidi mazoezi, epuka vyakula vya mafuta na makopo, jizuie kadiri uwezavyo kupiga punyeto labda mpaka uzidiwe sana.

4. Uko kwenye kipindi cha kuingia ukubwani, kwahiyo akili ya kiutu uzima inafunguka, hii hali huja na side effects kama za mama mjamzito. Hasira za ghafla, kukata tamaa, kulia au kutamani kulia, kuzira, kujitenga, kuwa mtu wa mawazo muda mwingi ni vitu visivyoepukika.

Hapa ndipo unapojishape kuwa wewe wa kesho, kwahiyo jitahidi sana yanapokutokea haya usiyaendekeze, vijana wengi huwin na kushindwa hapa. Ukiyapuuza na kusonga mbele mafanikio yako yataanzia hapo, utayachukulia kuwa ndio sehemu ya maisha yako, kushindwa kwako kutaanzia hapo.

Kama bado uko below 30 usiangalie mwili ulionao bali jipange kwa kuwa hii ndio hatua muhimu ya kuwa wewe wa kesho. Mustakabali wako umeubeba mwenyewe.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad