Siwezi Kumsamehe Mke Wangu, Ametembea na Mkurugenzi wa Ofisini Kwake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Baada ya kupoteza kazi yangu niliyumba sana, niliwaza nitaishije bila kazi hapa mjini, hata hivyo nilijipa moyo kwamba kwa kuwa wife ana kazi Basi mambo madogo madogo hayatasumbua wakati huo nami nitakua nakazana kutafuta kazi nyingine.


Kumbe nilikua nimekosea kuwaza hivyo, ilianza taratibu kama mzaha wife kuchelewa kurudi na kuja kuanzia saa tano usiku na kuendelea kwamba wamelazimika kufanya overtime.


Baada ya wiki kadhaa visingizio vikaisha akawa hana cha kusingizia tena, anakuja usiku ule ule mwingi bila kunisemesha chochote na kupitiliza chumbani kulala moja kwa moja bila kula wala kuoga.


Nikajiuliza, kwa biologia ya wanawake ilivyo na joto la Dar inawezekana wife akarudi na kulala tu bila kuoga? Na chakula je ina maana analala na njaa? Nikasema nitapata tu majibu ya maswali Haya, only time will tell.


Hadi napoteza kazi yangu sikua namiliki Gari wala wife hakua nalo, baada ya hizi harakati za kurudi usiku mwingi na kutoshinda home weekend nzima hatimaye wife """"" akanunua Gari""""" Toyota IST.


Nilikua naumia rohoni kwa suspicion but sikujua where and how to start investigation on that particular matter hadi siku moja tulienda pamoja na wife kwenye Gari lake na mdogo wake wa kike aliyekuja toka Jana yake.


Mimi niliomba nikae nyuma wao mbele, kabla hatujaondoka nashangaa kuiona chupi ya wife bikini pembeni ya miguu yangu ndani ya Gari, kwa kifupi ile safari ilikufa.


Nilimtoa ndani ya Gari kwa kipigo kikali sana nikitaka kujua kulikoni hiyo chupi kuwepo humo, hakawa hana cha kujitetea, nikamfungua chumbani na nikachukua simu zake zote nikawa nazo sebuleni, tangu kufunga ndoa sikuwahi kumpiga zaidi ya siku hiyo.


Hapo sebuleni nilipitia meseji zote kwenye simu zake, baada ya zoezi hilo nililidhika beyond reasonable doubt my wife was seeing someone else.


Na mtu huyo alikua ni mkurugenzi wake kazini, na hiyo kampuni anayofanya wife ni ya huyo bosi, nikamfungulia saa tatu usiku na kumpa simu zake nikaendelea na mambo mengine.


Sikupata usingizi siku hiyo, nilikaa kwenye TV nikibadilisha Chanel mbali mbali, saa nane usiku alinifuata sebuleni na kupiga magoti akaniomba msamaha kwa machozi kwamba hatorudia, haelewi kwa nini alifanya vile, sikumjibu nikamwambia arudi alale.


Nika conclude kwamba sina mke, nikaazimia kwamba nisilete fujo, kwa hali niliyonayo nijifanye -- tu huku moyoni nikijua sina mke, halaf niendelee ku fight nikifanikiwa niachane nae niendelee na maisha yangu.


Wife ali pretend kwamba ametubu na ameachana na yule jamaa, lakini kwa siri aliendelea nae, hakujua kama mimi najua yule mpenzi wake ndie bosi wake kazini, alikua amenidanganya kwamba ni mteja wa kampuni yao na kwamba hawaonani tena.


Kunipumbaza, kwa mara ya kwanza, ilikua ni Ijumaa, akaja na bahasha akanipa ilikua na million mbili za elfu kumi kumi, kaniambia amepata kazini baada ya kufanya deal, nikazipokea nikaziweka benki, Ili kuni fool kila siku mbili tatu au wiki alikua ananiletea pesa, laki tano na kuendelea nami nikawa natunza pesa nikikusanya mtaji.


Nikaanza kufanya shughuli zangu za kibiashara, kidogo kidogo mambo yangu yamekua mazuri kwa pesa hizo hizo za uzinzi wa wife, yeye kwa kipindi chote anaamini kwamba amenifanya --, akienda kulala kwa hotels na huyo jama, wakati mwingine akiaga anakwenda safari kikazi kumbe yupo humu humu Dar, nami nikajifanya mjinga nikajiimarisha.


Kila jambo lina mwanzo na mwisho, mkurugenzi kapata msichana mpya kazini inaonekana mke wangu katemwa, yupo tu nyumbani namuacha hapo asubuhi naenda kwa business zangu narudi jioni, nikimuuliza kulikoni analia tu, yupo frustrated, ndipo nikapata chanzo kikanieleza yaliyotokea huko kazini kwao, mapenzi na bosi yamefikia mwisho.

AJIRA: Nafasi Mpya za Kazi Serikalini, NGOs na Makampuni Binafsi.....Bofya Hapa kutuma maombi


Nimeishi kwa mateso rohoni kwa miaka 4, huku nikificha hasira yangu, nikishiriki tendo la ndoa, ili kumhadaa huyu mzinzi bila yeye kujua, sikuwahi kupata wazo la kufumania kwa kua nilikua nitaharibu mpango wangu.


Wiki hii najiandaa kuhamia kwangu ingawa ni vyumba viwili na sitting room but it is my home, naenda kuanza upya

Nasamehe mtoto pia, nitapata mwingine, kwanza sina imani kama ni wangu, nitaondoka na begi tu.


Yote Tisa, kumi nimepona rohoni, nasikia amani sana.


Kusamehe ni msamiati kwangu kwa sasa, hatua hii niliipanga miaka minne nyuma.


Ama kweli poteza kazi ndo utajua sura halisi ya mkeo
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad