Huyu Dereva Tax Atanivunjia Ndoa Yangu, Nifanyeje?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nimekuja kwenu nahitaji ushauri, ni urgent.

Hapo katikati niligundua kuwa Mr wangu ana kimada, tukasumbuana na kugombana sana juu ya hilo, ingawa sikumshika live ila ni wazi kwamba alikua nae, mbali na hilo pia ni mlevi kupindukia.

Nilipoona suala hilo linaendelea nikaona isiwe tabu, nikatafuta suluhisho.

Na mimi nikatafuta mtu pembeni aniliwaze, kuna dereva tax huwa tunamtumia sana kwa shughuli za kifamilia,
Nikaamua kumzawadia penzi huyo jamaa, sio kwamba nilimuanza mimi, bali alikua akinisumbua siku nyingi, hivyo nikaona nimkubali.

Katika mara zote nilizokutana nae (6) niligundua kwamba hajiwezi kabisa, nikaona this relationship is not worth it, nikampiga chini, pia mtu mwenyewe hana hata Chumba cha kulala, Mara zote anaazima Chumba kwa mwenzie, ingawa ukimuona kwa nje ubrazamen alionao huwezi amini, ni type ya wale wanaume wenye kuongea sana na mbwembwe nyingi lakini hamna lolote.

Nikakata mawasiliano nae na kumwambia asinitafute tena, akaanza kunililia nisimwache, anapiga simu muda wote kunibembeleza, kila akiniona hata na watu wengine Mtaani, labda Dukani n.k atakimbia haraka kuja na kuomba tuongee pembeni hadi kero.

Hivi karibuni nimepata mtu mwingine mahali nakoabudu, he is so caring, ni mtu mwenye Upendo sana, hanywi pombe na ananipenda kwa dhati, he is god fearing and above all his performance is much better than my husband and the tax driver's.

Juzi kumetokea shida kubwa baada ya Mr kushika sms ya yule tax driver akiendelea kunibembeleza, Nikalazimika kusema kuwa jamaa ndio ananifuatilia, ananitaka kimapenzi, akasema kama ni kweli na ili aniamini Basi tufanye fumanizi la kutengeneza, kwamba nikubaliane na yule kijana wa tax kwenda nae guest na yeye aje atufumanie na kundi la mabaunsa wamwoe wote.

Nikikataa mpango huo basi atajua nilishatembea nae, na mimi najua yule tax driver kwa vyovyote vile atauvaa huo mtego, namuonea huruma sitaki apate aibu hiyo wakati tulishaachana nae.

Nipo njia panda naombeni ushauri nifanyeje?
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Very wicked minded soul ukimfanyia hayo huyo basha wako cab driver ujue kuna siku moja na wewe utakuja kulipa hapa hapa duniani unajifanya mcha Mungu kumbe underground ni malaya mbovu una mumeo then a cab driver huridhika ukaona uwe na mtu mwingine wa 3 je mpaka mwaka huu uishe utakuwa umepandwa na wanaume wangapi?Huna mpango mwanamke asiyeuthamini utu na mwili wake kama mwanamke mksmilifu anavyotakiwa awe sasa hapo anaadhirika nani kati yenu mumeo au wewe?Of course wewe unaonekana "Cheap"

    ReplyDelete
  2. Kwa kuwa wote wewe, mumeo na huyo taxi driver ni wazinifu, hakuna haja ya wewe kujiongezea zigo jingine la dhambi, we mpe huo mchongo wote huyo taxi driver, kisha asafiri kwa muda wa miezi kadhaa, atangaze dharura aende kwao,tena akutumie sms ya kukuaga umwoneshe mumeo, akirudi kwao atakuwa amekoma na hadithi yenu itaishia hapo....

    ReplyDelete

Top Post Ad