AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Daktari wa Azam FC, Dr. Mwanandi Mwankema, anayeshughulikia taratibu za matibabu ya Mwantika amesema kuwa beki huyo anaendelea vizuri na matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
“Tunamshukuru Mungu David anaendelea vizuri na matibabu na yupo kwenye hatua za kuruhusiwa kurejea nyumbani baada ya kupata nafuu kutoka kwenye tatizo lililompata juzi,” alisema.
Mwantika alizimia dakika ya 64 na kupatiwa matibabu ya awali kabla ya kukimbizwa Hospitali ya Mbagala Zakhem na kuhamishiwa Hospitali ya Wilaya ya Temeke, na baadaye Muhimbili (MNH) ambako anaendelea kupata matibabu.
Aidha Dkt. Mwanandi amesema taratibu zinazofanyika kabla ya mchezaji huyo kuruhusiwa ni kufanyiwa uchunguzi wa moyo ili kufahamu kama ana tatizo hilo kwaajili ya matibabu zaidi.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK