Kenyatta Atia saini sheria ya makosa ya mtandaoni Ambapo Faini yake ni Milioni 100 Ukikutwa na Hatia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametia saini mswada wa Sheria ya Uhalifu wa Kompyuta na Mtandaoni ya mwaka 2018 kuwa Sheria, hatua hii itatoa adhabu kali kwa watakaopatikana na makossa ya mtandaoni.

Sheria hiyo inatoa adhabu ya faini ya Milioni 100 (dola 50,000 za Marekani) au kifungo cha miaka miwili jela, au adhabu zote mbili, kwa atakayepatikana na kosa la uenezaji wa habari za uzushi.

Mtu atakayepatikana na kosa la kueneza taarifa ambazo zinaweza kuzua taharuki au kuzua vurugu atafungwa jela zaidi ya miaka kumi.

Hatua hiyo imepokelewa kwa hisia na maoni tofauti kwa watu mbalimbali ambapo kiongozi wa zamani wa chama cha wanasheria Kenya Apollo Mboya amenukuliwa na vyombo vya habari akisema kifungu hicho kinaweza kuwapa watawala ‘uhuru’ wa kukandamiza vyombo vya habari.

Kwa upande mwingine shirika la kimataifa la kutetea uhuru wa wanahabari Committee to Protect Journalists (CPJ) nalo limekuwa likipinga uidhinishaji wa mswada huo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad