Kocha Kim Poulsen Aachia Ngazi Timu ya Vijana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kocha Kim Poulsen Aachia Ngazi Timu ya Vijana
Kocha Kim Poulsen ameamua kuachia ngazi timu ya vijana, ambapo alikuwa mshauri wa timu za vijana nchini kufuatia kukumbana na changamoto mbalimbali licha ya kufanya kazi hiyo kwa kipindi kirefu.

Kim ambaye amekuwa msaada mkubwa ndani ya timu za taifa za vijana hapa nchini ajira ambayo alipewa na Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) ameamua kuachia ngazi nafasi hiyo ambayo ameitumikia tangu mwaka 2016.

Kim Poulsen ambaye ni raia wa Denmark ameanza kazi hapa nchini akiwa kocha mkuu wa timu za vijana mwaka 2011 na kupandishwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa (Taifa Stars) mwezi Mei mwaka 2012 aliporithi mikoba ya Jan Poulsen.

Licha ya mkataba wa Kim kukatishwa mwaka 2014 ulipofika mwaka 2016 akawa mshauri wa ufundi kwa kushirikiana na aliyekuwa kocha wa Serengeti Boys, Bakari Shime na kuiwezesha Tanzania kucheza fainali za Afrika ikiwa ni kwa mara ya kwanza nchini Gabon mwaka 2017.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad