AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Yanga inaenda kucheza mechi hiyo ikiwa na kumbukumbu za kwenda suluhu tasa ya 0-0 dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda ambayo wapo nayo kundi moja (Kundi D), mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi ya keshio itawapasa Yanga kuhakikisha wanapata ushindi kujiwekea mazingira ya kusalia kwenye michuano hiyo ambapo hivi sasa bado wana alama moja pekee katika msimamo wa kundi hilo.
Ikumbukwe Yanga ilipoteza dhidi ya MC Alger kwenye kibarua cha kwanza pia suluhu dhidi ya Rayon na kuwafanya kuwa kwenye mazingira magumu kunako kundi D.
Dawa pekee ya Yanga kujipa matumanini ni kuhakikisha inawafunga Gor Mahia kesho kisha kuanza maandalizi mengine ya mchezo wa mkondo wa pili utakaopigwa Dar es Salaam.
Yanga itashuka dimbani bila wachezaji wake mabeki Hassan Kessy na Yondani ambao imeelezwa wamebaki Dar es Salaam wakihitaji kuongezewa mikataba mipya.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK