Yanga Yamalizana na CAF.... Yakamilisha Usajili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Yanga Yamalizana na CAF.... Yakamilisha Usajili
Kaimu Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga, Omary Kaaya, ameanika hadharani orodha ya wachezaji ambao usajili wao ulikuwa haujakamilika katika Shirikisho la Soka Afrika (CAF).


Kaaya amewataja wachezaji hao kuwa ni Matheo Athony, Mkongomani Herieter Makambo pamoja na Deus Kaseke ambaye alisajiliwa kutokea Singida United.

Yanga imefanikisha kukamilisha usaili wa wachezaji hao ambapo Makambo ameongezeka baada ya kukosekana katika mchezo uliopita dhidi ya Gor Mahia uliofanyika Jumapili ya Agosti 29 jijini Dar es Salaam.

Wakati Makambo akiongezeka kwenye orodha ya wachezaji ambao usaili wao CAF umekamilika, kikosi kipo mjini Morogoro hivi sasa kiiendelea na mazoezi. Yanga imepiga kambi ya wiki mbili kujiandaa na mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya USM Alger utakaopigwa Agosti 19 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad