AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na MCL Digital wakili wa Makene, Fred Khiwelo amesema jeshi la polisi linaendelea kumshikilia kwa ajili ya uchunguzi kuhusiana blog iitwayo Chadema.blogspot.com pamoja na maudhui yake.
“Ni kweli nimemfuatilia mteja wangu kujua haki ya kupata dhamana baada ya kushikiliwa toka jana lakini polisi wamesema wanaendelea na uchunguzi na hivyo hawawezi kutoa dhamana kwa muda huu,” amesema Khiwelo.
Amesema swala la kumiliki mtandao mwanachama yeyote anaweza kuwa anamiliki kwa jina hilo, kumshikilia mteja wake kwa muda wote bila kumpa dhamana ni ukiukwaji wa sheria.
Mchana wa leo, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema akizungumza makao makuu ya Chadema amesema jeshi la polisi linaendelea kumshikilia Makene.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK