Mpaka Mwanamke Anaamua Kuchepuka Ujue Kuna Shida kwa Mumewe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Katika Utafiti wangu imegundua kuna tatizo kubwa katika mahusiano aidha ya kimapenzi au ya ndoa.Uaminifu umekuwa tatizo kubwa miongoni mwa jamii ya kizazi hiki! Kutoridhika imekuwa sehemu ya maisha ya sasa si kwa mwanaume au mwanamke kuchepuka ndiyo habari ya mujini kwa sasa hadi wale walioaminika kuwa viongozi wa dini maana hakuna mwenye kinga ya kutotenda dhambi hivyo imekuwa kujitwalia kadri tupendavyo nani atakuwa kiini cha mabadiliko katika wimbi hili linaoelekea kupoteza wengi.

Tatizo ni nini hasa kwa uzoefu wangu wa kuishi katika dunia hii na katika ndoa kwa muongo zaidi ya mmoja nimegundua mwanamke anaweza akatulizwa (walioko ndoani) tu endapo mume atakidhi mahitaji yote ya kiuchumi,zaidi kuwa na muda wa kutosha na mkewe bila kusahau kusaidiana kufikishana katika kilele cha maraha ambacho.Mungu aliona ni vema atupe wanadamu kama kitulizo ktk maisha yetu haya yenye adha nyingi.

Sasa cha ajabu kuna baadhi ya wanaume wamekuwa busy wakiamini magari,pesa na fahari ndiyo vitaziba uhitaji wa mke katika kukidhi haja ya upendo ndiyo maaana lawama haziishi watu wanachapiwa na kuishia kulalama eti wanawake hawaridhiki hata uwape nini mwanamke haswa alilyelewa vyema akihudumiwa bed na akapata mahitaji ya kiuchumi sina cha kufata nje hata kidogo.

Nina zaidi ya miaka 13 ya ndoa hivyo najua nisemacho sioni fahari wala sijawahi kufikiria kutoka na mtu nje ya mume wangu kwa muda wote huo ila kuna mazingira baadhi wanaume wanasababisha hadi mke unajiona mhitaji,mume hashikiki ndani kila siku kuja home late mvivu kitandani hayuko romantic nk unategemea mke afanyeje?

Ilihali naye ana damu inachemka(hapa siharalishi kuchepuka ila mke anakuwa katika upweke mkuu nani ampe faraja mpaka mke anaamua kutoka nje kuna tatizo kubwa hivyo chukueni tahadhari waume wenye tabia hizi zinajeruhi sana mioyo yetu (nasi tunapendwa sana huko nje uwezo wa kutoka kama mnavyotoka tunao sana..ila ni staha tu na hofu kwa Mungu muumbaji.Wanaume many sehemu yenu na wanawake pia ili tuishi kwa raha bila kuumizana.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad