Mzee Mwingine Anayetibu kwa Kikombe Kama Babu wa Loliondo Aibuka Dar

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mzee mwingine anayetibu kwa kikombe kama babu wa Loliondo aibuka Dar
Mamia ya watu wa jiji la Dar es salaam jana Septemba 13, 2018 wamemiminika katika eneo la Feri kupata tiba baada ya mtu mmoja aliyeibuka na kutangaza kuwa anagawa dawa ya asili ambayo inatibu maradhi yote.

Mganga huyo aliyejitambulisha kwa jina la Jacob Kawawa ameliambia gazeti la Nipashe kuwa anauza dawa hiyo kwa Tsh 3,000/= na vipimo vyake ni tofauti na vile vya mzee wa Samunge ambaye alikuwa anatumia kikombe.

Kawawa amesema yeye anatumia chupa ya maji ya lita moja, ambapo mpaka sasa watu wenye maradhi mbalimbali ikiwemo kisukari, kansa na magonjwa mengine wameshapona kabisa, kupitia tiba yake.

Mashuhuda walioongea na gazeti la Nipashe, wamesema kuwa Mganga huyo alianza kutoa tiba hiyo katika eneo la Feri mwezi mmoja uliopita na hakupata wateja wengi, lakini kadri siku zinavyozidi kwenda wateja wanazidi kuongezeka na wengine wakitoa ushuhuda.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad