Mwili wa Khashoggi Ulicharangwa Vipande Baada ya Kuawa ili Kupoteza Ushahidi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwili wa Khashoggi Ulicharangwa Vipande Baada ya Kuawa ili Kupoteza Ushahidi
KWA mujibu wa ofisa mmoja wa serikali ya Uturuki asema mwili wa mwanahabari, Jamal Khashoggi, ulicharangwa vipande baada ya kuawa ili kupoteza ushahidi

Khashoggi alionekana akiingia ndani ya Ubalozi wa Saudi Arabia tarehe 2 mwezi huu na hakuonekana tena baada ya kuingia katika jengo hilo la ghorofa sita.




Inaelezwa kuwa watu waliomfanyia mahojiano Jamal na hatimaye kumuua walipewa maagizo na mtoto wa Mfalme wa Saudi Arabia, Mohammed bin Salman.


Mwandishi huyo alijikita katika kufichua maovu ya utawala wa kifalme wa Saudi Arabia kupitia kazi yake ya uandishi wa habari






Habari nyingine zinasema Khashoggi alikuwa anatuhumiwa kuwa na uhusiano na utawala wa Qatar ambao una uhasama na ufalme wa Saudi Arabia.


Wakati watu wengi duniani wakitaka kujua kilichomfika Khashoggi, jana (Jumanne) Rais Trump wa Marekani na Waziri wa Mambo ya Nje, Mike Pompeo, wamesema Saudi Arabia imewajulisha kwamba uchunguzi juu ya tukio hilo umeanza na majibu yatatolewa karibuni.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad