AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
RC Makonda ametoa onyo kali kwa yeyote atakayeibuka na kuanza kusambaza taarifa za uongo kuhusiana na tukio hili au kuligeuza na kulifanya mtaji wa kisiasa.
Amesema msemaji wa tukio hili kwa upande wa polisi ni Kamanda wa Kanda Maalum Dar Lazaro Mambosasa na kwa upande wa Serikali ni yeye.
Katika hatua nyingine,Makonda, amependekeza kufungwa kwa kamera katika maeneo yote jijini Dar es salam, ili kupata msaada mkubwa yanapotokea matukio ya kiuhalifu kama hili.
Amesema iwapo Dar es salaam itafungwa kamera, itakuwa msaada mkubwa kwa vyombo vya usalama kufuatilia matukio ya kiuhalifu kama la kutekwa kwa Mo Dewji.
“Tuna mpango mkubwa zaidi nafikiri umefika wakati sasa wa mkoa wa Dar es salaam wote kufungwa camera, leo hii tungekuwa na camera, tungeongezea hata weledi wa jeshi letu la Polisi kufuatilia gari iko wapi, ifike hatua Dar es salaam iwe na camera tukamate wahalifu kwa haraka zaidi, kuliko kutumia nguvu kubwa kumfuatilia mtu ambaye hujui amepita wapi”, amesema Paul Makonda.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Mipango mingi ikipangwa na hasa miundo mbinu masuala ya ulinzi na usalama usaulika, ingekuwa wadau wote wanashirikishwa kila mdau muhimu angetoa ushauri wake muhimu. Hapa uangaliwa ni tajiri yupi na anawekeza nini na nani anahusika na uwekezaji huo basi.
ReplyDelete