AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mbali na kuthibitisha tarehe, Simba pia imetangaza kuandaa utaratibu wa mashabiki wake wanaotaka kusafiri kwenda nchini Zambia kuiunga mkono timu yao kwenye mchezo huo.
''Tumeandaa utaratibu wa Safari kwa njia ya barabara ambapo nauli ni shilingi laki moja na elfu thelathini (130,000) kwenda na kurudi, kutokea Dar es Salaam hadi mjini Kitwe na safari itaanza Alhamisi Alfajiri na kufika huko Ijumaa jioni'' imeeleza taarifa ya klabu.
Pamoja na nauli hiyo, msafiri pia anapaswa kuwa na hati ya kusafiria inayokidhi matakwa ya kisheria na Hati ya chanjo ili aweze kusafiri kwenda Zambia.
Simba inakutana na Nkana Red Devils baada ya kuitoa Mbabane Swallos kwa jumla ya mabao 8-1 katika michezo miwili ya raundi ya awali ya michuano hiyo. Simba ikivuka hatua hii inaingia katika hatua ya makundi.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK