Marekani Ikitengeneza Makombora na Sisi Tutatengeneza- Rais wa Urusi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Marekani Ikitengeneza Makombora na Sisi Tutatengeneza- Rais wa Urusi
Urusi itaunda makombora yaliyopigwa marufuku chini ya mkataba wa vita baridi ikiwa Marekani itajiondoa katika mkataba unaodhibiti silaha hizo, ameonya rais Vladimir Putin.

Tamko lake linakuja baada ya shirika la kujihami kwa mataifa ya magharibi Nato, kuilaumu Urusi kwa kukiuka mkataba wa makubaliano kudhibiti uundaji wa makombora ya masafa ya kadri (INF).

Makubaliano hayo yaliyotiwa saini mwaka 1987 kati ya Marekani na USSR,yalipiga marufuku mataifa hayo yote mawili dhidi ya kuunda makombora ya masafa mafupi na yale kadri.

Rais wa Putin amesema tuhuma za Nato dhidi ya taifa lake ni kisingizio cha Marekani kujiondoa katika mkataba huo.

Katika tamko hilo lililoangaziwa kwenye televisheni, kiongozi huyo alisema mataifa mengi yanaunda silaha zilizopigwa marufuku katika mkataba wa INF

"Sasa inaonekana kuwa washirika wetu Marekani wanahisi kwamba mambo yamebadilika sana kiasi cha kuwa wanaonelea ni lazima wao pia wawe na silaha ," alisema.


Rais wa Marekani Donald Trump siku za hivi karibuni aligusia kuwa taifa hilo huenda likajiondoa katika mkataba huo kutokana na mienendo ya Urusi.

Wadadisi wanasema Urusi unachukulia suala la uundaji wa silaha hizo kama mbinu mbadala ya kuimarisha vikosi vyake na gharama yake ni nafuu.

Alipowasili kwa mazungumzo na mawaziri wa mambo ya nje wa EU, Kiongozi wa muungano wa Ulaya anayesimamia sera za nje Federica Mogherini ametoa wito kwa mataifa hayo mawili kudumisha mkataba huo akiongeza kuwa "Umekuwa hakikisho la amani na usalama barani Ulaya kw amiaka 30 sasa".

Katika taarifa shirika hilo lilisema: "Washirika wa wote wamekubaliana kuwa Urusi iliunda kombora aina ya ,9M729 ambayo inakiuka mkataba wa INF katika hatia ambayo inatishia usalama wa muungano wa Euro-Atlantic".

Taarifa hiyo pia ilisema kuwa nchi wanachama wa muungano huo"zinaunga mkono" madai ya Marekani kwamba Urusi ilikiuka mkataba huo, na kuitaka Moscow "kuchukua jukumu la kuutekeleza kikamili".
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad