AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Simba itakuwa ugenini kucheza na Nkana Jumamosi na marudio yanatarajiwa kuwa Desemba 23 au 24 Dar es Salaam katika Uwanja wa Taifa.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Katibu wa Simba, Dr. Arnold Kashembe, alisema kuwa maandalizi ya timu yapo sawa na wanatarajia kuondoka kimafungu kwa kuwa kuna wengine ambao wameshatangulia kuweka mipango sawa huku wengine wakifuata kuungana nao baadaye.
“Mpaka sasa tumeshatambua kuwa aina ya timu tunayokwenda kucheza nayo ni ngumu, hivyo tumedhamiria kupata matokeo mazuri, kwa kuanza safari yetu tunajigawa makundi kufika Zambia kwa kuwa hatuwezi kwenda wote kwa wakati mmoja.
“Taratibu zote zipo sawa na uhakika wa kufanya vizuri ni mkubwa na ndiyo maana kuna watu ambao wametangulia kuanza kufanya maandalizi kwa ajili ya timu yetu, kuhusu kuondoka kwa wachezaji na viongozi utaratibu utakuwa wazi hivyo Watanzania na mashabiki sapoti yenu muhimu,” alisema Kashembe.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK