Chura Mpweke Duniani Apata Mchumba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Chura Mpweke Duniani Apata Mchumba
Chura anayeaminika kuwa wa mwisho wa aina yake katika ulimwengu ameondolewa upweke.

Romeo, anayejulikana kama chura wa pekee ulimwenguni, ameishi miaka 10 ya kutengwa katika hifadhi ya Bolivia.

Wanasayansi wanasema wamempatia mchumba kwa jina Juliet baada ya safari ya kwenda msitu wa Bolivia.

Chura watano wa majini walipatikana katika vidimbwi vya maji na kukamatwa, kwa kusudi la kuzalishana na kupandikiza upya wanyama hao kwenye pori.

Teresa Camacho Badani ni mkuu wa kitengo cha viumbe hai katika hifadhi asili iliyopo Cochabamba na kiongozi wa safari hiyo.

Anatarajia kwamba vyara hao wa jinsia tofauti watapaendana: "Romeo ni mtulivu na hana mizunguko," aliiambia BBC. "Romeo ana afya na anapenda kula, lakini ana aibu na mpole."

Juliet, hata hivyo, ana utu tofauti sana. "Yeye ana nguvu sana, huogelea sana na anakula sana, wakati mwingine anajaribu kutoroka."

Vyura watano - wanaume watatu na wanawake wawili - ni vyura wa kwanza wa maji kuonekana katika pori kwa miaka kumi, licha ya utafutaji uliofanyika katika jangwa la Bolivia.

Romeo alichukuliwa miaka 10 iliyopita wakati wanabiolojia walipojua aina hiyo ya chura ilikuwa katika shida, lakini hakutarajiwa kubaki peke yake kwa muda mrefu.

Wafanyakazi kulazimishwa wakapumzike Korea Kusini

Alivutia hisia za mataifa mwaka mmoja uliopita juu ya kutafuta kwake mwenzi, na hata alipewa kurasa katika mtandao wa kutafuta mpenzi.

Vyura waliopatikana hivi karibuni wametengwa katika hifadhi ya makumbusho, ambapo huko wanapambana kuhakikisha viumbe hao wanabaki hai.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad