AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Saa tano kamili asubuhi akisindikizwa na maafisa wa bunge Pof. Assad ameingia bungeni kisha kujiandikisha katika kitabu cha wageni kabla ya kuingia ukumbi wa mahojiano saa 5 na dakika sita ambako alihojiwa hadi saa 8:47 mchana.
Akizungumza na wanahabari baada ya mahojiano ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka, Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Mbunge wa Tabora Mjini, Emmanuel Mwakasaka amekiri kwamba CAG amehudhuria mahojiano na kutoa ushirikiano mkubwa hivyo mapendekezo yatapelekwa kwa spika Job Ndugai.
Januari 7, 2019 Spika Job Ndugai alimtaka CAG kufika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhojiwa kutokana na kauli yake ya aliyoisema akiwa nje ya nchi kwa kusema kuwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni dhaifu.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK