Nguo zinazofanana na sare za JWTZ zanaswa kambi ya wakimbizi Kigoma

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nguo zinazofanana na sare za JWTZ zanaswa kambi ya wakimbizi Kigoma
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, imekamata nguo zinazofanana za sare za kijeshi katika makambi ya wakimbizi.

Akizungumza na waandishi na kamati hiyo mjini hapa jana Alhamisi Januari 10, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Samson Hanga, alisema nguo hizo zilikamatwa Desemba 31 mwaka jana kati ya saa tano asubuhi hadi sita mchana kwenye  makambi ya wakimbizi.

“Jumla ya nguo zinazofanana na sare za kijeshi 1,947 zilikamatwa katika kambi ya wakimbizi ya Mtendeli na Nduta zote za hapa hapa Kigoma.

“Katika Kambi ya Nduta zilikamatwa sare 1,325 na Mtendeli 622,” alisema.

Pamoja na mambo mengine, alisema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea ili kuwabaini walioingiza sare hizo na lengo lao.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad