Serikali Uganda yaweka sheria kali kuwabana wasanii wa muziki, marufuku kulewa, kuvaa mlege/nguo fupi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Uganda yaweka sheria kali kuwabana wasanii wa muziki, marufuku kulewa, kuvaa mlege/nguo fupi jukwaani
Serikali ya Uganda kupitia Wizara ya Utamaduni na Sanaa imetangaza sheria mpya zenye lengo la kuwabana wasanii, ili kulinda maadili na sanaa kwa ujumla.


Sheria hizo ambazo zimetangazwa wiki iliyopita, zinaeleza kuwa msanii yeyote hawezi kwenda nje ya nchi hiyo kutumbuiza bila kibali .

Moja ya sheria mpya, ni kwamba Msanii yeyote wa muziki hatakiwi kupanda jukwaani akiwa amevaa nguo fupi au mlegezo.

Sheria nyingine, msanii hataruhusiwa kupanda jukwaani kutumbuiza akiwa ametumia kinywaji au kilevi chochote.

Mabadiliko hayo pia, yanamtaka kila msanii asajiliwe na haitaruhusiwa wimbo uachiwe bila kukaguliwa na mamlaka husika ya serikali.





Hata hivyo, mabadiliko hayo yamepelekea baadhi ya wasanii akiwemo Eddy Kenzo kuandaa mikutano ya kushinikiza sheria hizo zilegezwe
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad