Tundu Lissu Apigiwa Kampeni ya Urais

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Jesca Kishoa amesema zawadi pekee ambayo Watanzania wanaweza kumpa mbunge wa chama hicho jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu ni kumuunga mkono katika ndoto zake za kugombea urais mwaka 2020.


Kishoa ametoa kauli hiyo leo Januari 14, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali kuhusu afya na maendeleo ya Lissu.

“Lissu ni kaka yangu, ni mbunge mwenzangu na kiongozi wangu, mambo ya kuangalia ni kupata baraka za chama lakini anafaa,” amesema Kishoa.

Amesema wakati ukifika atatamani kuona jina la Lissu likipitishwa kuwania urais, kwa kuwa Watanzania wanajua msimamo wa kiongozi huyo na ndio anayefaa kuwaongoza.

Lissu kwa sasa anaendelea na ziara yake kwenye nchi za Ulaya na marekani kwa ajili ya kuelezea mkasa wa kupigwa risasi uliompata Septemba 2017 Jijini Dodoma.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ili aiuze nchi yetu?!
    Anatumika ujue!!

    ReplyDelete
  2. Aiuze mara ngap ?????
    Mbona ilishaga uzwa kitaaaambo??????

    Labda ailipie deni il tuwe huru.


    Hata kama akitumika ni bora kuanza nae...kuliko kucha...

    ReplyDelete

Top Post Ad