AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msemaji wa Simba SC, Haji Manara amesema kipigo walichokipata dhidi ya As Vita ni cha aibu ila kwa sasa wanatulia na kutafakari.
Haji amesema hayo ni matokea mabaya kwao lakini wanaelewa kuwa ni mpira wa miguu na ni mashindano makubwa.
"Sasa cha kufanya Kwanza tutulie tutafakari wakati benchi la ufundi na uongozi ukiangalia chakufanya. Tutulie bado tuna mechi nne, mbili nyumbani na nyingine mbili ugenini," ameeleza Haji Manara.
Tayari Simba SC wanarejea kimya kimya bila kishindo kufuatia kuambulia kipigo kizito cha goli 5-0kutoka kwa AS Vita. Kwa matokea hayo hadi sasa Simba SC wanasalia na pointi zao tatu walizozipata kwenye mchezo wao wa mwanzo dhidi ya JS Saoura kutoka Algeria.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK