Manara autaja Mwezi Atakaoacha kazi Simba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Baada ya kusambaa kwa tetesi nyingi kuwa Afisa Habari wa Simba, Haji Manara yuko mbioni kutemwa katika nafasi yake, mwenyewe ameibuka na kueleza kinagaubaga kuhusiana na taarifa hizo.


Tetesi hizo zilisambaa mara baada ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Simba Sports Club, Mohamed Dewji 'Mo' kuitisha mkutano na wanahabari, Ijumaa Februari 8 kuhusiana na masuala mbalimbali ya klabu hiyo pamoja na maandalizi ya mchezo wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Al Ahly.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Manara amesema kuwa anafahamu kuwa mashabiki wengi hasa wa Yanga wanapenda asiendelee kuwepo Simba na siku wakisikia ameondoka watamfanyia sherehe kutokana na jinsi anavyowatesa.

"Kuna watu wa Yanga hamu yao nife kabisa!!, nawaumiza sana na siku mtakaposikia sipo kikazi Simba, mtafanya sherehe. Ila nikuhakikishie kuwa Mungu akinipa uhai nitaacha kazi Januari 2021 tena kwa hiari", amesema Manara alipokuwa akijibu 'comment' ya moja ya mfuasi wake.

Pia tetesi za Simba kuachana na Manara zimezidi kutiwa chumvi hasa pale Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi alipotangaza ujio wa nafasi za kazi katika idara mbalimbali hivi karibuni, ambapo watu wenye taaluma hizo watatuma maombi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad