Msanii maarufu nchini Nigeria, Banky W afuata nyayo za Professor Jay na Sugu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Muigizaji, Muimbaji wa muziki na Mjasiriamali maarufu nchini Nigeria, Banky W ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Eti-Osa, Lagos nchini humo.

Banky W ametangaza nia hiyo kupitia chama cha Modern Democratic Party (MDP) ambapo ameahidi kuboresha huduma za jamii ikiwemo elimu.

Akihojiwa na kituo cha runinga cha CNN, Banky W amesema kuwa “Kuna kundi kubwa la vijana nchini humo wanaongea na Ku-Tweet sana mitandaoni lakini hawachukui maamuzi. Kitu ambacho kinarudisha nyuma maendeleo ya taifa la baadae. Nataka niwafundishe vitendo na kuwaelimisha namna Demokrasia ya kisasa inavyoweza kufanya kazi na kutengeneza Nigeria ya baadae,“.

Banky W anakuwa msanii mkubwa wa muziki nchini humo kujitosa kugombea Ubunge nchini humo.

Tayari wasanii wenzake, kama Davido amejitokeza hadharani kumpigia upatu kwenye uchaguzi Mkuu ujao Februari 16, 2019 .

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad