Mwigulu Nchemba aeleza sababu za ukimya wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwigulu Nchemba aeleza sababu za ukimya wake
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amesema kwa sasa amekuwa kimya kutokana hayopo tena kwenye nafasi hiyo, hivyo amekuwa na vitu vichache vya kusemea.

Ameeleza hayo kwenye mahojiano na kipindi cha Clouds 360 kinachoruka Clouds TV amesema kwa sasa amekuwa zaiddi jimboni kwake.

"Unajua ukiwa kwenye nafasi ya uwaziri vipo vitu vingi vya kuvisemea, ndio maana sasa hivi nipo kimya nimebaki na vitu viwili tu vya kusemea mambo ya jimboni kwangu na kazi nzuri inayofanywa na serikali yangu," amesema Dkt. Mwigulu.

Ameendelea kwa kusema, 'Hakuna tofauti na maisha yangu hayajabadilika, nilipokuwa waziri kwenye msafara wangu sikutaka magari yasimamishwe ili nipite, kwa sababu kuna wengine walikuwa wanawahi ndege "airport', wengine wagonjwa na wengine makazini sikutaka kuwachelewesha,'.

Utakumbuka July 2018 Rais John Magufuli alifanya mabadiliko madogo katika baraza lake la Mawaziri, ambapo ameteua Kangi Lugola (aliyekuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira), kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Mwigulu Nchemba.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad