AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Aliyasema hayo kwa waandishi wa habari wakati akiwa njiani kurejea kwenye makaazi yake akirejea katika safari yake ya kihistoria huko Abu Dhabi.
Hata hivyo ,Papa alisema kwamba Vatican na wanachama wengine wa jumuiya ya kimataifa wangehitaji kuchukua hatua za awali kabla ya kuanza mchakato wa majadiliano.
Papa Francis alitanabahisha pia kuwa ameipokea barua kutoka kwa Maduro lakini alisema hajaisoma:
'Kabla ya ziara yangu, nilitambua kuwa rais wa Venezuela Nicolas Maduro ametuma barua na alikuwa ametuma barua katika kikapu cha kidiplomasia'.
'Nakiri bado sijaisoma barua hiyo, tutaona nini cha kufanya, ni muhimu sana' alisema.
Kwa hali ilivyo inapaswa pande zote mbili ziombe upatanishi wa kimataifa kama ilivyo wahi kutokea kwa nchi za Argentina na Chile.
Papa anachokiona nchini Venezujela kilikuwa sehemu ya majadiliano, yaliyofanyika kati ya Zapatero na Monsinyori Sheri na baadaye kuendelezwa na askofu Celli.
Kutoka huko alizaliwa kiumbe mdogo, hakuna moshi.
Sasa, sijui: nitaifungua barua hiyo baada ya hapo nitaangalia cha kufanya, lakini hali ya awali inahitaji kuwa pande zote mbili zitake suluhu.
Nchi ya Venezuela raia walio wengi ni wa madhehebu ya dini ya kikatoliki, wanaogopa kwamba msimamo kati ya bwana Maduro na kiongozi wa mpito Guaido unaweza kushuka katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Guaido, ambaye anaungwa mkono na serikali ya Marekani na washirika wake, alijitangaza kuwa rais wa kipindi cha mpito wiki mbili zilizopita, akimshtaki raisi aliyekuwa madarakani Nicolas Maduro kwa ukiukaji wa taratibu za uchaguzi wa mwaka jana.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK