AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Katika chapisho la Twitter , bwana Trump alitangaza kwamba milima hiyo ni muhimu sana katika usalama wa Israel na uthabiti wa eneo la mashariki ya kati.
Israel iliunganisha milima hiyo na taifa lake hatua ambayo haikuungwa mkono na jamii ya kimataifa.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ambaye ameonya kuhusu Iran kuingilia vita vya Syria alituma ujumbe wa shukran kwa bawana Trump kupitia mtandao wa twitter.
''Katika wakati ambapo Iran inataka kuitumia Syria kama eneo la kuikabili Israel, Bwana Trump aliitambua Israel kama mmiliki rasmi wa milima ya Golan.
Richard Haass, afisa mwanadamizi katika wizara ya kigeni nchini Marekani ambaye ndiye rais wa baraza la uhusiano wa kigeni alisema kuwa hakubaliani na bwana Trump.
Alisema kuwa hatua ya kuitambua Israel kuwa mmiliki wa milima hiyo ni ukiukaji mkubwa wa azimio la Umoja wa Mataifa , ambalo linapinga unyakuzi wa eneo moja kupitia vita.
Uamuzi huo wa rais unajiri wakati ambapo Netanyahu anakabiliwa na ushindani mkali katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu tarehe tisa mwezi Aprili mbali na msururu wa madai ya ufisadi.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK