AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa daktari huyo, raia wa Cameroon, aliuawa kwenye mji wa mashariki wa Butembo hapo jana.
Mkuu wa shirika hilo, Tedros Adhanon Ghebreyesus, amethibitisha kifo cha mfanyakazi huyo kupitia ujumbe wake wa Twitter.
Meya wa mji wa Butembo, Sylvain Kanyamanda, amesema mauaji yalifanyika kwenye Kliniki ya Chuo Kikuu ya Butembo, akiwatuhumu waasi wa kundi la Mai-Mai kuhusika.
Mashambulizi dhidi ya wafanyakazi wa huduma za afya kwenye eneo hilo, ambalo WHO inasema limeshapoteza watu 751 kwa Ebola, yamekuwa yakifanyika mara kwa mara
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK