Tahadhari Kutoka Jeshi La Zimamoto Na Uokoaji Nchini Kuhusu Kimbunga Kenneth

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kutokana na utabiri uliotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) kuhusu kutokea kwa Kimbunga kikali (KENNETH) na mvua kubwa leo tarehe 25 Aprili 2019 kitakachoathiri maeneo ya Pwani ya Kusini mwa nchi na kusababisha madhara mbalimbali. Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linatoa rai kwa Wananchi wote waishio katika maeneo hatarishi, maeneo yaliyopo pembezoni mwa bahari na kandokando ya Mito, kuchukua tahadhari katika kipindi hiki kwa kuyahama maeneo hayo haraka.

Wananchi wanatahadharishwa kuchukua tahadhari katika kipindi hiki na kuendelea kufuatilia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka Hali ya Hewa Tanzania na kusikiliza vyombo vya habari pamoja na kuzingatia tahadhari zinazotolewa, ushauri na miongozo ya kitaalam ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

Tuchukue tahadhari kwa kuepuka kukaa au kuegesha vyombo vya Usafiri na Usafirishaji chini ya miti mikubwa, maana matawi au mti vyaweza kuangukia chombo na kusababisha uharibifu mkubwa wa Mali hata kudhuru Maisha.

Kutokana na Kimbunga hiki kikali kinachoambatana na mvua kubwa kuna uwezekano wa mawe makubwa au udongo kuporomoka kutoka milimani au miti kuanguka na kuziba barabara, hivyo madereva wanapaswa kuwa makini kwa kuendesha vyombo kwa mwendo unaokubalika ili kuepuka ajali zisizo za lazima.

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limejipanga na liko imara kuhakikisha linatoa huduma bora, sahihi na kwa wakati.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad