Aunt Ezekiel Aandika Waraka Mzito Kuhusu Sakata la Kuachana na Iyobo "Msinifundishe cha Kufanya mnataka Nipige Puchu?"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MSANII wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel ameamua kufunguka na kuweka wazi kuhusu wanaomsema kufuatia kuachana na mzazi mwenzake, Mose Iyobo.



Kupitia ukurasa wake a Instagram, Aunt ameandika waraka mzito kuhusu sakata hilo huku akiwatolea povu ile mbaya watu wanaomtukana mitandaoni kutokana na uamuzi wake wa kuachana na Iyobo na kuchukua mwanamme mwingine.



Habari zenu? Naitwa Aunty Ezekiel (Mama Cookie), nimeona niaongee hili ili kuwa nafasi ya kila mmoja muendelee na kazi zenu maana naona leo kuna wengine mmeacha yenu kabisa kama kawaida wajuzi watoa nasaha Washauri wa Instargam, mnaojua maisha kushinda mtu yoyote yule, mnaojua kuna kudharirika kushinda wenye maisha yao.



Bana natamani mjue tuu labda kama kuna wageni humu kwa wenyeji naomba mfahamu mimi sifundishwi maisha plz plz plz, endeleeni na yenu msinifundishe cha kufanya, najidharirisha kuwa na bwana mwingine mnataka nipige Puchu?



Bwana angu niliyenaye shoga alilala na baba akoo! Halafu naomba ikumbukwe haya ni Maisha yangu Mm na Familia yangu sio ya kwenu.



Hata hayo Mnayoyaona now mliyapenda ni mimi ndio nilifanya myapende, mlianza hivyo hivyo, so plz naomba tu niwakumbushe THIS IS MY LIFE. Na hayo mnayotamani niyaongee sitakaa niongee, kwa taarifa yenu mimi nimefundwa sijatoka juu ya miti, nimelelewa siwezi muongelea mtu aliyenipeleka labour hata iweje.



Maana haya majina hayawezi kubadilika, tutabadilika sisi na mahusiano yetu, sio hili jina la huyu mtoto plz… msipende kugombanisha watu nyie hamtaki watu waachane kama nani khe! Tufe na majanga ya kuvumiliana ndani kisa Instagram watanionaje?



Huo  upuuzi sijafanya, bado naishi maisha yangu nitakayo sio mtakayo nyinyi, nina maisha yangu, ana maisha yake hayo ni makubaliano yetu nyinyi yanawahusu nini?

Looh! hebu plz bana, mnataka watu hadi siku wasisalimiane ndio huwa mnaona utamu! PUMBAVU, hebu naomba mniache plz…. Nina mtoto anaejua kuchezea simu na siku moja atakuwa atayakuta, mnataka anichukulie vipi?



Naomba mniache na haya yote nafanya course of My Baby Girl na sio mwingine yeyote. Msije mkajipa imani eti nitaona haya oooh mara kujidharirisha, mama zenu wabadili mabwana sisi tukibadili tunajidharirishaa, Aaah kina mwajuma vipi babuuu.

Hebu tufunge huu mjadala mnalotaka hamtalipata kwangu, endelea ku-enjoy na picha kutoka nyanda za juu kabisa nikiwa na haka kamarioo au kashoga toka Zanzibar, kwangu mimi ka-handsome boy, nite nite, mtazoeatuu!



-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad