Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesitisha ubadilishaji wa fedha za Kenya, ili kukabiliana na uingizwaji wa fedha haramu nchini. Hatua hiyo pia ni kuitikia wito wa Benki Kuu ya Kenya (CBK), ambayo imewataka wenye fedha za Kenya kwenda kuzibadili nchini humo ili wapate noti mpya.