AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
“Ujue kwa kipindi kirefu Mondi alikuwa nchini Ufaransa na madansa wake pamoja na meneja wake, Sallam SK akitengeneza video yake ya Inama aliyomshirikisha Fally Ipupa. “Alipokuwa nchini humo alipata nafasi ya kwenda kumtembelea Eto’o nyumbani kwake,” kilisema chanzo na kuongeza;
AONESHWA MAKOMBE
“Baada ya kufika akiwa na Sallam walipewa misosi ya nguvu na mwisho wa siku akaoneshwa makombe yake tofauti ikiwa ni sehemu ya mafanikio yake tangu ameanza soka.“Makombe hayo yalikuwa ni pamoja na matatu ya UEFA aliyoyapata akiwa na vilabu tofauti.”
MONDI ALIPA
Hata hivyo, Mondi alitumia mwanya huo kumkaribisha Eto’o nyumbani kwake, Mbezi-Beach jijini Dar baada ya kusikia amealikwa kuwa mgeni rasmi katika mashindano maalum ya mpira wa miguu. “Wakiwa Mbezi-Beach, Mondi alihakikisha Eto’o anakula vyakula vya Kibongo na mwisho wa siku naye akampeleka kuangalia mafanikio yake kwenye muziki ambapo alimuonesha tuzo zake nyingi zilizopangwa kwenye kabati maalum ambazo alizipata ndani na nje ya nchi kwa nyakati tofauti.
“Baada ya yote kupita, Mondi alimsikilizisha baadhi ya nyimbo zake na mwisho kabisa wakaelekea eneo la kucheza pool table na kuanza kucheza,” kiliweka nukta chanzo hicho.
ETO’O AMPIGIA SALUTI
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Eto’o aliweka picha aliyopiga na Mondi na kuandika; “Kutoka Paris (Ufaransa) hadi Dodoma (alichanganya kidogo alikuwa akimaanisha Dar es Salaam). Asante sana kwa kunipatia chakula usiku wa jana.
“Najisikia faraja kuwa na kaka wanaofanya vitu vya tofauti Afrika. Ubarikiwe kwa huduma yako nzuri.” Mondi naye aliingia katika komenti hiyo na kujibu; “Kaka natumaini umependa chakula cha Kibongo.”
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK