Mwanamuziki Alikiba Akubali Kubadilishana na Wafaransa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 
Msanii wa Bongofleva Alikiba, amefanya mazungumzo na balozi wa Ufaransa Frederic Clavier leo Juni 17, 2019, ambapo wamekubaliana mambo mbalimbali ikiwemo kuendelea kubadilishana utamaduni.


Alikiba amethibitisha mchongo huo leo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instgram ambapo amendika, ''Mapema asubuhi ya leo nilipata fursa ya kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini - His excellence Frederic Clavier ofisini kwake''.

Akiweka wazi mazungumzo yao, amefunguka haya, ''Tumezungumza mengi kuhusu namna gani tunaweza kujenga daraja la kubadilishana utamaduni baina ya Tanzania na Ufaransa''.

Alikiba ni miongoni mwa wasanii ambao huenda wakawa wanafahamu kidogo lugha ya Kifaransa ambapo amewahi kuimba baadhi ya mashairi yake kwa Kifaransa katika wimbo wake wa Aje.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad