Paul Makonda si Mchezo, Atimiza Ahadi yake Kwa klabu ya Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ametimiza ahadi yake aliyoahidi siku ya hafla ya kuichangia klabu ya Yanga maarufu kama ‘KUBWA KULIKO’ ambapo aliahidi kuipatia uwanja klabu hiyo.

Makonda amekabidhi nyaraka za uwanja huo uliopo Kigamboni jijini Dar es salaam kwa mwenyekiti wa klabu hiyo. Mshindo Msola na kuwahakikishia umiliki halali wa uwanja huo.

Akizungumza baada ya makabidhiano hayo, Makonda amesema kuwa makabidhiano hayo yanatoa ishara nzuri kwamba serikali ina nia ya dhati ya kukuza michezo.

”Jumamosi iliyopita niliahidi kuwa nitaipa klabu ya Yanga uwanja eneo la Kigamboni na leo tumeanza mchakato wa kuwamilikisha rasmi ili waanze ujenzi wa uwanja wao,”amesema Makonda

Kwa upande wake kaimu katibu mkuu wa Yanga, Omary Kaaya amemshukuru mkuu wa mkoa na serikali kwa ujumla kwa kuwapatia uwanja huo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad