AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
RC Makonda amesema utaratibu wa kushiriki Shindano hilo ni Wahusika kwende kwenye sehemu za Bar,Saloon,Vijiwe vya bodaboda na Sokoni kisha kuwahoji wananchi waeleze namna wanavyoifahamu jumuiya ya SADC na kurusha mahojiano hayo kwenye platform zao ambapo pia wananchi watakaoweza kutoa majibu kwa ufasaha nao watapatiwa kiasi cha shilingi Laki moja.
Aidha RC Makonda amesema Mshindi wa kwanza wa shindano hilo atapatiwa kiasi cha Shilingi Milioni 3, Mshindi wa pili Milioni 2 na Mshindi wa tatu Milioni 1 ambapo hafla ya kukabidhi zawadi hizo itafanyika August 05 mwaka huu.
Hata hivyo RC Makonda amewataka Wamiliki wa Platform za Social Network kudhihirishia jamii kuwa mitandao yao ina uwezo mkubwa wa kubadilisha jamii kama ikitumika vizuri ambapo kwa kufanya hivyo watazidi kuheshimika na pia kuingiza pesa kupitia matangazo.
Huu ni mkakati wa RC Makonda kuendelea kuboresha maisha ya vijana waliojiajiri na kuajiri wenzao kupitia mitandao ya kijamii akiamini kupitia mitandao hiyo wanaweza kupata kipato kikubwa na serikali ikapato kodi.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK