Serikali ya Botswana kupinga uamuzi wa mahakama kuu uliohalalisha mapenzi ya jinsia moja

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali ya Botswana itaka rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama kuu nchini uliohalalisha mapenzi ya jinsia moja, mkuu wa sheria amesema.

Mwezi uliopita mahakama hiyo ilipinga sheria za wakatiwa ukoloni zinazotaja kifungo cha hadi miaka saba gerezani kwa yooyte anayejihusisha katika mapenzi ya jinsia moja, ikieleza kwamba sheria hiyo inakwenda kinyume na katiba.

Uamzui huo ulipongezwa na wengi na kutajwa kuwa ni kupiga hatua katika kuimarisha haki za wapenzi wa jinsia moja Afrika.

'Kwa nini vita dhidi ya mapenzi ya jinsia moja haiishi'
Aifichua siri ya firauni
Ni kwanini picha hii ya Malala inashutumiwa?
Lakini mkuu wa sheria nchini humo Abraham Keetshabe amesema majaji katika mahakama hiyo wamefanya makosa.

"Nimesoma kwa kina uamuzi huo wa kurasa 132 na maoni yangu ni kwamba mahakam kuu ilifanya makosa katika kufikia uamuzi huu," Keetshabe amesema katika taarifa iliyotolewa jana Ijumaa.

Ameongeza kwamba ataipeleka kesi hiyo katika mahakama ra rufaa, lakini hakutoa ufafanuzi zaidi kwa misingi ya rufaa hiyo.

Haki miliki ya pichaEPA
Uamuzi wa mahakama kuu mwezi uliopita ulifikiwa kwa pamoja na majaji watatu.

" Utu wa binadamu unapata madhara wakati makundi ya walio wachache yanabaki nyuma," Alisema Jaji Michael Leburu alipokuwa anasoma hukumu . " Jinsia ya mtu si mtindo wa fasheni. Ni utambulisho wa maana wa utu."

Kesi iliwasilishwa na mwanafunzi aliyelalamika kwamba jamii imebadilika na mapenzi ya jinsia moja yanakubalika katika maenoe mengi.

Hukumu hiyo ilipokelewa kwa shangwe kubwa na wanaharakati wanaoendesha kampeni za wapenzi wa jinsia moja kote barani Afrika, ambako mahusiano ya mapenzi hayo ni kinyume cha sheria za nchi nyingi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad