Trump: Marekani imeidungua ndege isiyo na rubani ya Iran

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Raisi wa Marekani Donald Trump amesema jeshi la maji la Marekani limetungua ndege isiyo na rubani ya Iran katika eneo la mpaka kati ya ghuba ya uajemi na ghuba ya Oman.

Amesema meli ya jeshi lake ''ilichukua hatua'' siku ya Alhamisi baada ya ndege hiyo kusogea kwa takriban mita 914 karibu na chombo hicho.

Iran haijasema chochote kuhusu hilo. Mwezi Juni, Iran iliangusha ndege ya kijeshi isiyo na rubani ya Marekani, na kusababisha hofu ya kutokea mzozo wa kijeshi.

Awali Tehran ilisema imekamata ''meli ya kigeni'' na wafanyakazi wake 12 siku ya Jumapili kwa kusafirisha mafuta kinyume cha sheria.

Iran imekuwa ikishutumiwa na Marekani kwa kushambulia meli zake tangu mwezi Mei.Tehran ilikana shutuma hizo.

Haki miliki ya pichaEPA
Raisi Donald Trump amesemaje?

Akizungumza Ikulu, Trump amesema ''Ninataka kuwajulisha kuhusu tukio lililotokea kwenye eneo la mpaka wa Hormuz leo lililohusisha meli yetu ya kijeshi.

Chombo hicho kilichukua hatua ya kujilinda dhidi ya ndege isiyo na rubani ya Iran ambayo ilikuwa karibu sana hatua iliyokuwa ikitishia usalama wa meli na waliokuwa ndani ya meli hiyo. Ndege hiyo iliharibiwa mara moja''.

Hili ni tukio miongoni mwa matendo mengine ya uchokozi unaofanywa na Iran dhidi ya meli zinazokuwa kwenye maji ya kimataifa. Marekani in haki ya kujitetea, na kutetea maslahi yake''.

Washington awali ilisema Iran lazima haraka iachie meli ambayo ilidai kushikiliwa na Iran.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad