Wananchi watahadharishwa na Mamlaka ya dawa za kulevya kuhusu vitafunwa vya mtaani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Jamii imetakiwa kuwa makini na vitafunwa vinavyouzwa mitaani, ikiwamo keki na kashata kwakuwa kumeibuka mtindo mpya wa kuchanganya bangi na dawa nyingine za kulevya.

Akizungumza katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), maarufu Sabasaba, ofisa kutoka Kikosi cha Kuzuia Dawa za Kulevya (Adu), Sajenti Chad Ngatunga, alisema kadiri siku zinavyokwenda, watumiaji wa mihadarati wamekuwa wakitumia mbinu mpya ili kutenda uhalifu.

Alisema watumiaji wa mihadarati hiyo wanafahamu maeneo wanayouziwa bidhaa hizo zilizochanganywa na dawa.

“Wapo wengine wanakwenda duka la madawa wananunua dawa kisha wanahangaika na kimiminika aina ya Energy na kujikuta wakilewa kupitiliza,” alisema Ngatunga.

Alisema mabadiliko ya sheria yaliyofanyika mwaka 2015 kuhusu bangi na dawa za kulevya yameongeza adhabu za matukio hayo ili kukomesha vitendo hivyo ndani ya jamii.

 “Mabadiliko ya sheria kwa sasa yamebadilika, hivyo kwa anayekamatwa na dawa za kulevya gramu 20 anaweza kufungwa maisha au adhabu kali na akikutwa na bangi kilo 50 anazuiwa dhamana,” alisema Ngatunga.

Alisema mwaka huu kuna binti alikwenda kumtembelea rafiki yake wa kiume, hakumkuta, akaangalia ndani ya friji na kukuta keki akala, lakini ilikuwa na dawa za kulevya.

“Baada ya kula ile keki akaanza kulegea na kukimbizwa hospitali,  polisi walipopewa taarifa wakafika eneo la tukio na wakaichukua keki hiyo, ilipopimwa walibaini ilichanganywa na dawa za kulevya,” alisema Ngatunga.

Alisema utafiti mdogo walioufanya wamebaini watu wengi hawana uelewa kuhusu dawa za kulevya na athari zake.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad