Watekwaji Waambiwa Waseme Ukweli Wanaowateka ni Kina Nani ili Tunusuru Wengine

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu hapa nchini (THRDC), umetoa rai kwa wale wahanga wote wa utekwaji, wanapotoka hadharani na kuongea na umma waeleze kinagaubaga kilichowakuta, ili kuondoa sintofahamu miongoni mwa watu wengi.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa Mtandao huo Onesmo Olengurumwa, wakati akitoa tamko la kuhusu matukio ya upoteaji na utekwaji, na kutoonekana kwa watu yanayoendelea hapa nchini, ambapo amesema matukio haya yanaleta taswira mbaya ndani na hata nje ya nchi.

''Inaweza ikawa inachangia na kuwapa wale watu, wanaofanya utekaji nguvu zaidi, kwamba tunaowateka hata tukiwaachia hawaendi kusema chochote, tuanawasihi sana mnapopata fursa ya kurudi ni vyema ukaongea yale yote yaliyokusibu, na kuweza kuwapa moyo na nguvu watu ya kupiga kelele'', amesema.

Aidha Olengurumwa, ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wabunge wake waingilie kati suala hili, na wao walisimamie ili mwisho wa siku waje na maadhimio ya kuona ni namna gani suala hili litaisha.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad