AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kamanda wa Polisi kanda Maalumu ya Rufiji Onesmo Lyanga, amethibitisha kutokea kwa ajali ya ndege ndogo ya shirika la Tropical, iliyokuwa ikiruka kutoka katika kiwanja cha ndege cha Mafia kuelekea Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi kanda Maalumu ya Rufiji Onesmo Lyanga.
Kamanda Lyanga amesema ajali hiyo imetokea leo Agosti 6 majira ya saa 4:00 asubuhi, baada kuanguka na kuteketea kwa moto na ilikuwa na abiria takribani tisa.
''Ndege imepata ajali ilikuwa inaruka uwanja wa Mafia kwenda uwanja wa Julius Nyerere Dar es salaam, ilikuwa na watu 9 lakini mpaka sasa hivi hakuna aliyefariki na kuna majeruhi 6 na ndege yote imeteketea.
Aidha kamanda amesema kuwa majeruhi wote 6 wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu zaidi na kwamba Jeshi la polisi Mkoani humo linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK