Mahakama yamwongezea hukumu Baba Levo Ahukumiwa Mwaka mmoja Jela

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 
Diwani wa Mwanga Kaskazini (ACT-Wazalendo) Manispaa ya Kigoma Ujiji, Clayton Chipando maarufu Baba Levo ameongezewa kifungo kutoka miezi mitano jela hadi mwaka mmoja.

Hukumu hiyo imetolewa leo Septemba 10, 2019 kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma, baaada ya kushindwa rufaa yake ya kupinga hukumu ya awali.

Baba Levo alikata rufaa katika mahakama hiyo kupinga adhabu ya awali ya miezi mitano, kwa kosa la kumshambulia trafiki, F.8350 PC Msafiri Mponela.

Katika hukumu ya awali Baba Levo alitiwa hatiani kwa kifungu namba 240 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 chapisho la mwaka 2002 na hukumu yake kutolewa Alhamisi Agosti 1, 2019, katika mahakama ya Mwanzo Mwandiga na Hakimu Mkazi Florence Ikolongo.




-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad