ATCL Yasitisha Safari Zake Afrika Kusini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL) limesitisha rasmi safari zake kati ya Dar es Salaam na Johanessburg, Afrika Kusini,  kuanzia Oktoba 7, 2019, na abiria ambao tayari walikuwa wamekata tiketi kwa ajili ya usafiri huo watarudishiwa nauli zao.



Taarifa iliyotolewa na ATCL Oktoba 3, 2019, na kusainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Ladislaus Matindi,  iliwaelekeza mawakala wa tiketi wote kurejesha nauli za wateja hao ambao tayari walikuwa wamekata tiketi.



ATCL ambayo ilikuwa ikifanya safari hiyo mara nne kwa wiki (Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumapili) iliacha kufanya safari kati ya miji hiyo Agosti 23,2019 baada ya ndege yake aina ya Airbus A220-300 kuzuiliwa katika uwanja wa Oliver Tambo jiji Johannesburg kwa amri ya Mahakama Kuu ya Guateng.



Baada ya takribani wiki mbili ndege hiyo iliachiwa huru kwa uamuzi wa mahakama.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad