CHADEMA wapata pigo tena mwenyekiti mkoa wa Njombe ajiunga na CCM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa wa Njombe na Mwanasheria Wa kutegemewa Kwenye Kesi ya Emmanuel Masonga Ya Kupinga Ushindi WA Mbunge Mwalongo Mkoa Ndg, Edwin Swalle amekihama Chama hicho na Kutangaza Kujiunga na Chama Cha Mapinduzi Leo October 06/2019

Tukio limefanyika katika Ofisi za CCM Wilaya ya Njombe.

Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wa pili mkoa wa Njombe Edwirn Enosy Swale (wakili) baada ya wa awali ndugu Fakih Lulandala kukihama chama hicho mwaka 2018 na kujiunga na chama cha mapinduzi naye pia hii leo amejiuzulu uenyekiti wa chama hicho na kujiunga na CCM.

Akizungumza mara baada ya zoezi la kupokelewa,kuapishwa na kukabidhiwa kadi ya chama cha mapinduzi katika ofisi za CCM wilaya ya Njombe amesema amefanya maamuzi hayo kutokana na juhudi zinazofanywa na Rais Magufuli katika kuleta maendeleo nchini.

“Mimi kama kijana nimeamua kwa dhati kutumikia nchi yangu katika chama ambacho kwa sasa kimekuwa na muelekeo wa kusaidia wananchi,na nitoe wito kwa vijana wote nchini na watanzania kwa ujumla wake,tusije tukapoteza fursa ya kutokumtumia Magufuli kuipeleka nchi yetu katika hali neema”alisema Swale

Katika hatua nyingine chama cha mapinduzi kimempokea aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la vijana (BAVICHA) jimbo la Lupembe Msafiri Peter Mpolo,ambaye amesema ameamua kuhama chama hicho kutokana na kuto kuwepo kwa ajenda za kusimamia kwa sasa.

“Tumeona hakuna sababu ya kuendelea chama cha upinzani kutokana na mambo makubwa ambayo yamefanywa na serikali kwa sasa,ukienda Makete utaona barabara zinavyojengwa,watumishi wamekuwa na nidhamu kubwa,hizo ndio ajenda tulizokuwa tunasimamia lakini leo hii nikibaki Chadema nitasimamia nini”alisema Msafiri Peter Mpolo

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha na kuwakabidhi kadi wanachama hao mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Njombe Edward Mgaya,amemtaka Swale kuunganisha nguvu zake pamoja na mbunge wa jimbo la Lupembe Jorum Hongoli ili kufikisha maendeleo katika jimbo hilo
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad