Nilivyofanya Bonge la Sherehe Baada ya Mke Wangu Kufukuzwa Kazi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Huyu mke nilimuoa akiwa hana kitu, kwa bahati alitafutiwa kazi na ndugu yake kwenye kampuni moja ya simu akawa analipwa kama milioni 3 kwa mwezi fasheni na yeye yeye na fasheni vipodozi kila aina,handbag na nywele za laki mbili ndio mshahara wake ukawa unaishia huko mimi mshahara wangu hauzidi laki sita,nilifanyishwa vituko vyote ndani ya nyumba ,manyanyaso yote ,hapiki hafui,hafanyi chochote ndoa ikawa inaelekea kuvunjika.

Nikaenda mahakamani kuprocess talaka wakasema mpaka nianzie baraza la usuluhishi la kata au kanisani,nikaamua kwenda kanisa tulilofungia ndoa tukaitwa kwa Baba Paroko for hearing sijui mediation sijui arbitration sijui mie nikatinga kwa bajaj ya kukodi nimepaukaaa yeye akaja na RAV4 .
Baba Paroko alivyotusikiliza akaaniita pembeni akasema kijana hapa nadhani hata tukiomba na kukariri mistari yote ya biblia plus mapambio yote ndoa yako haitarudi kama mwanzo pambana utafute hela ,huyu ni mchaga katumwa pesa mjini

Nilisali sana nikasugua goti nikamuomba Mungu mara mambo yangu yakakaa sawa mshahara ukawa mara mbili plus marupurupu anagalau . baada ya miezi miwili sina hili wala lile mara simu yangu nilishangaa mke wangu kunipigia mchana ,tumeachishwa kazi kmpuni imeuzwa,hureeeeee niliruka ruka kwa furaha sana nikapigia simu washikaji tukaenda kunywa bia na nyama choma mpaka saa sita usiku kabla polisi na makonda hawajatuvamia nilijua ile kazi ndio inaniharibia ndoa na aliipata kibahati hawezi tena kupata kazi kama ile.

Hela yote ya NSSF akajaribu kufanya kila biashara biashara zikabuma mtaji ukakata alijifanya hajui kupika sasa anapika kuliko hata wapishi wa Kempinski,alijifanya sijui hawezi kufua sasa anafua kuliko dobi ,kitandani alijifanya mvivu sasa yuko vizuri kuliko wacheza shoo wa fally ipupa ,RAV4 imepaki tu muda wote ananilelea watoto kwa nini nisimshukuru Mungu

Funzo:
Wanawake Msijisahau sana pale mnapokuwa vizuri kifedha zaidi ya mume
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad