Nyota Mwingine Aongezwa Katika Kikosi cha Taifa Stars

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

BEKI wa kati wa Azam FC, Oscar Masai, ameongezwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kilichoingia kambini jana.

Stars imeingia kambini kujiandaa na mechi mbili, ya kwanza ikiwa ni ya kirafiki na Rwanda 'Amavubi', itakayopigwa  Kigali, Oktoba 14, pamoja na ile ya marudiano ya kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Sudan Oktoba 18.

Masai, ni beki chipukizi, alikuwa na kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana 'Ngorongoro Heroes' kilichotwaa ubingwa wa vijana wa CECAFA wikiendi iliyopita.

Wachezaji wengine wa Azam FC walioitwa kikosi hicho ni Nahodha Msaidizi, Frank Domayo 'Chumvi', Mudathir Yahya, Salum Abubakar 'Sure Boy', Idd Seleman 'Nado' na mshambuliaji Shaaban Chilunda.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad