Waziri Mkuu Awamwagia Sifa DC,DED wa Ikungi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri Mkuu awamwagia sifa DC,DED wa Ikungi
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewapongeza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Justice Kijazi kwa kuamua kuchapa kazi na kuweka mbele maslahi ya wananchi.

“Moja ya Hamashauri zilizotulia ni Ikungi. Hii ni Halmashauri pekee ambayo Mkuu wa Wilaya ya Mkurugenzi wake wanaongea lugha moja. Endelezeni kazi hii nzuri ili viongozi wengine waje kujifunza kwenu,” alisema na kuamsha shangwe miongoni mwa watumishi waliohudhuria mkutano wa hadhara.

Alitoa pongezi hizo, wakati akizungumza na wananchi na watumishi wa Halmashauri hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Ikungi.

Aliwataka watumishi wa Halmashauri hiyo watambue kwamba wako chini ya wananchi na kwamba bila ya uwepo wao, hata wao wasingepata kazi wilayani humo. “Mimi na ninyi sote ni watumishi wa hawa wananchi. Bila wao, tusingekuwa na utumishi hapa. Lazima mtambue kwamba mmeletwa hapa ili muwahudumie wao,” alisisitiza.

“Nendeni vijijini, wahudumieni bila kujali umri wao, dini, rangi au itikadi zao. Wakiuliza masuala ya kilimo au maji au afya, washughulikieni na muwape majibu huko huko. Wananchi wengine wanaishi vijiji vya mbali na hapa, wengine hawana nauli, wengine hawajui hata wakija mjini waanzie wapi,” alisisitiza.

“Nimekuwa nikisisitiza kwamba wakuu wa idara wasikae ofisini kwa wiki nzima. Nendeni vijijini mkawasikilize wananchi. Wakuu wa idara tofauti, jipangeni mtumie gari moja; siku nne kati ya tano za wiki, nendeni vijijini mkasikilize wananchi na siku mbili zilizobakia mje muandike taarifa zenu ofisini,” alisema.

“Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi simamieni hili, kwa sababu ni mojawapo ya matakwa ya Serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha wananchi wanahudumiwa ipasavyo.

Mapema, akitoa salamu, Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Edward Mpogolo alimweleza Waziri Mkuu kwamba uuzaji wa pamba katika wilaya hiyo unaendelea na hadi sasa wameshauza tani milioni 1.4 kati ya tani milioni 2.5 walizojiwekea malengo.

“Pamba imeendelea kununuliwa kwa bei ya sh. 1,200 kama ilivyoelekezwa na hadi sasa tani milioni 1.4 zenye thamani ya sh. bilioni 1.7 zimenunuliwa viwandani. Tunaishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuwawezesha wananchi hawa kupata fedha hiyo,” alisema.

Alisema anaishukru Serikali kwa kuboresha huduma za afya, mikopo kwa wanawake na vijana, umeme na elimu ambapo ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 64 hadi asilimia 83.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad