Papa Msofe afikishwa Mahakamani kwa utakatishaji Fedha, Uhujumu Uchumi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mfanyabiashara maarufu Marijan Msofe maarufu ‘Papaa Msofe’ na wenzake wanne wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka matano ikiwemo utakatishaji wa fedha wa zaidi ya TSh.Mil 900.

Mbali na Msofe, washitakiwa wengine ni Wakili wa Kujitegemea, Mwesigwa Mhingo,Fadhil Mganga, Wencelaus Mtui na Joseph Haule na miongoni mwa mashitaka yanayowakabili ni Kuratibu Genge la uhalifu,utakatishaji fedha na Kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Wakili mwandamizi wa Serikali Ladslaus Komanya amedai washtakiwa wanadaiwa kufanya makosa hayo kati ya Desemba 2018 na Septemba 2019 ndani ya Jiji la Dar es Salaam ambapo walijipatia zaidi ya Shilingi Milioni 900.
 
Washitakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu kesi hiyo ni ya uhujumu uchumi, hivyo haina dhamana ambapo shauri hilo limehairishwa hadi December 16, 2019.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad