Sad Story:Siwezi Wachukia Wanawake wote..Ila Wamenitenda Sana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mimi ni kijana wa kiume nina miaka 24, makazi yangu ni jijini mwanza,nimeamua kushea story yangu ili niweze kupata ushauri kwa watu mbali mbali juu ya nini nifanye baada ya kutendwa katika kila uhusiano ninao anzisha naweza nikasema nilichelewa kidogo kujihusisha na mapenzi kwa mujibu wa Dunia ya sasa,na hii ni kwa sababu nimelelewa na kukua katika familia yenye maadili.

Siwez nikasema nina mvuto mkubwa saana , niko simpo tu kama profile pictures zangu zinavyojieleza lakini siku zote nimejikuta nikiwa kipenzi cha kinadada wengi kulingana na mazingira husika ntakayokua nikiishi, na binafsi me ni mwanamume mtanashati naejpenda sana, mpole na zaid ni mcheshi haswa pengine hizo ndiyo sababu..na story yangu ya mahusiano inaanza nikiwa na miaka 20,kipindi nilipojiunga katika chuo kimoja hapa mwanza.

Baada ya kufika pale chuoni nilijijengea idadi kubwa tu ya marafi na kama unavyojua mtu mcheshi hua ana malafiki wengi ,pamoja na hayo, ckua na mawazo kabisa ya kuwa na msichana kimapenzi richa ya kua nlikua nina miaka 20,na kiukweli nilikua kama naogopa ogopa coz ckuwahi kabla richa ya kua wasichana wengi walikua wakijiweka karibu sana tu na wengi walihisi natoka nao au mmoja wapo..ila baada ya mda kuna mdada mrembo ambae nilimkuta pale chuoni alikua amenizd umri kama miaka 3 hivi,alitokea kunizoea sana,kama kunichukulia chakula.

kuja chumbani kwangu n.k hivyo akatokea kua mtu wangu wa karibu lakini kumbe alikua ananitaka kimapenzi na mwisho wa siku baada ya kua amenitamkia mwenyewe akaja kua galfriend wangu wa kwanza...kiukweli niliyafurahia sdana mahusiano yale,na yeye akawa ndiye mwalimu wangu katika mapenzi.

furaha yangu na huyo dada ilidumu kwa takribani miezi 9,na mambo yalikuja badirika alipokalibia kumaliza chuo, maana alikua
amenitangulia,kidogo kidogo vituko vikaanza mara hapokei cmu,hataki story na mimi,akitoka hataki tuongozane na anatoka akiwa ameupala kupita kiadi,kama mtu mzima kengere ya hatari ikaanza kugonga kua kuna kitu na pengine no more love tena.

Kiukweli nilikua naumia sana,sana tu,coz kuna kipindi alikua ananifokea hata mbele za class mates na ukizingatia mimi ni mpole sana,nilivumilia lakini mambo yalipozidi ikafika hatua nikasema NO,nami nikakata kamba baada ya kugundua kumbe alikua akimegwa na limtu lingine,hivyo nami nikajitahidi kukaa mbali nae ingawa nilikua naumia sana nimwonapo,na hatimae ukafika mda wao wa kufanya mtiani wa mwisho,ila kwa bahati mbaya yeye na baadhi ya wanafunzi walifutiwa mtiani kwa kosa flani kwenye chumba cha mtiani hivyo iliwabidi wabaki wfanye mtiani upya,na hawakuruhusiwa kukaa hostel za chuo,kiukweli nilimhurumia sana EX wangu ,coz ckua na kinyongo na nilikua bdo nampenda,nilimsaidia kumtafutia mahali pa kuishi akifanya mtihani na gharama zingine

Na kwa kipindi hicho alionyesha kubadilika sana ikawa kama mapenzi yameanza upya ila alipomaliza tu mtihani nyodo zikaanza,dharau na kuniumiza kimaksudi(wnawake!!!!)mpaka alipoondoka na mimi nika giv-up kabisaa (COZ MATUKIO NI MENGI CWEZI KUSIMLIA KILA KITU,NAOMBA NILUKE BAADHI YA MATUKIO NA NISIMLIE TU YALIYONIGUSA ZAIDI) ilipita miezi kadhaa nikiwa alone nisitake mwanamke kabisa ila nikaja kukutana na mdada mmoja tulokua tukisali nae -kanisani,nilimvutia,- alinivutia,tukaanzisha mahusiano, (HAPA KATI KATI YALIPITA MAMBO MENGI TU) lakini nikiwa chuoni tulikua tukiwasiliana vzuri tu lakini likizo moja nikiwa kwenye mtanda wa facbook,nikawa napitia plofile yake nikashaangaa kukuta plofile pics yake kuna pic ya mwanaume nasiemjua na relationship status yake inasomeka yumo in relationship na huyo mwanamume,nilimtafuta kujua kinachoendelea akasema ni kweli yuko na mwanaume mwingine ,kumuliza sababu akasema ameamua tu COZ HAWEZI KUA NA MWANAMUME WA KUPIGIANA CMU TU..na kama utani uo ndiyo ukawa mwisho na huu ukawa ni uhusiano wangu wa pili (RICHA YA KUA NILIKUA NI MWANAUME MWENYE MAPENZI HALISI,MWENYE KUJARI
NA KILA KITU ANACHOKIPENDA MWANAMKE) UHUSIANO WA 3:

huyu alikua ni mganda aliekua akisoma chuo jirani na nilichokua nikisoma mimi na nilikutana nae wakati wa maonesho yaliyohusisha vyuo vya maeneo yale,na moja ya maonesho yalikua ni onesho la mavazi na moja wa wahiriki toka chuo nilichokua nilikua ni mimi na siku mbili baada ya tamasha, nilipata friend request kadhaa kwenye facebook na mojawapo alikua ni mdada toka hicho chuo ..MWANZO NILIMPUUZIA SANA LAKINI CKU NDIYO NAMUONA BAADA YA KUPANGA TUONANE,CKUAMINI,NA CWEZI NIKAELEZEA NI KIASI GANI YULE BINT ALIKUA MREMBO,MREMBO HASWAA WA ASILI, so tukawa malafiki,na yeye kama alivyokua yule wa kwanza,alianza kunionesha ishara zote za kua urafiki wa kawaida cyo anao uhitaji,bali ni mapenzi na baada ya kupita mda kidogo nazani kwa kuona celekei aliamu kunifungukia yeye mwenyewe,kama waliotangulia alininiambia kua alinipenda siku nyingi tangu cku ile nimeonesha mavazi chuoni kwao na tangu kipindi hcho alipenda siku moja ajenge mahusiano na mimi..

Nazani hakuna mwanaume alie singo na Rijari then akakataa bahati kam hii,hivyo uhusiano mpya ukazaliwa,akawa msichana wangu wa 3 kimahusiano(SIKUA NAPENDA NA KILA NILIPOANZISHA UHUSIANO RENGO LILIKUA NI LONG TERM RELATIONSHIP BUT CKU ZOTE NILIKUA NIKIANGUKIA KWA GIRLS WASIYO SAHIHI) tulifanya mambo mengi SANA ya kufulahisha katika mapenzi KIASI KWAMBA HAKUKUA NA MWANYA WA KUFIKILIA KUA SIKU MOJA MWENZANGU ATAGEUKA,NA UKWELI KABISA RICHA YA KUA CKUA NA
CKU NYINGI KATIKA MAHUSIANO LAKINI NILIKUA NAJUA NINI MWANAMKE ANATAKA ,NINI NAPASWA NIFANYE NA WAPI NIMFANYE AWE NA FURAHA NA NILIKUA NINAWAPA REASONS ZA KUJIVUNIA KUA THEY GOT A REALY PERFECT MEN..

LAKINI baada ya miezi 5 ya uhusiano alianza kuwa tofauti..mawasiliano akapunguza..mara nyingi akawa hapokei simu zangu NA HATA AKIKUTA MICD CALL ZANGU HASHITUKI KABISA na nilipojaribu kumdadisi kulikoni,alinijbu kua yuko kawaida (NA MARA NYINGI ALIKUA AKINIJBU KUA"KWANI UNATAKA TUZUNGUMZE KUTWA NZIMA AU MMARA KWA MARA NDIYO UJUE KIASI GANI NAKUPENDA" )na zaid alikua akidai ni masomo tu yanamtait,,nilijilazimisha kumwelewa lakin sikulizika na hali ile.

Siku moja nisiyopenda kuikumbuka..na ambayo inaonesha ni kias gani kuna watu wameteswa na mapenzi....nakumbuka cku hiyo nilimtafuta nikawa namsihi abadilike,awe kama zamani coz sikutaka kabisa nimuache au tuacheni coz skua na mpango wa kua na girlfriend mwingine(kama nilivyotangulia kusema kua napenda kua na msimamo kwa msichana mmoja) ..aliniahid kua atabadilika na kwa kuanza akaniomba usiku nimpigie tuongee vizuri kam zamani kwani hata yeye aliyamis sana maongezi yetu matamu ya usiku..niliflahi sana nikijua furaha yangu inaenda kurud tena..na siku hiyo nilijiunga cheka ya 2000 kabisa ili tu maongezi yetu yasijekatishwa njiani.

Usiku wake nilimpigia akapokea lakini kwa sauti kama mtu asiyetaka mtu aliekaribu asikie,akaniambia kua nimtafute baadae,sikujari sana maana nilijua pengine anajisomea Na baada ya nusu saa nilimpigia tena,simu iliita sana pasipo majibu..kwa baadae ikipokelew lakini sauti
niliyoiskia sikuitalajia.. ILIK UA NI SAUTI YA MPENZI WANGU HUYO AKITOA SAUTI KAMA YA MTU ANAEFANYA TENDO LA NGONO msituko na maumivu niliyopata ni siri yangu na nilichofanya badara ya kukata simu,nilitoa kabisa battery ya simu na nikaiwasha kwa baadae wakati nikijaribu kuutafuta usingizi maana kawaida ya kuzima simu kwa mda mlefunikiwa na maumivu makari kabisa simu yangu ilianza kuita na mpigaj akiwa ni huyo mpenzi wangu,nilishtuka na sikupenda kuipokea ila baada ya kuita sana nilipokea na sauti niliyoiskia si ile niliyoitegemea,alikua ni mwanaume,AKINIONYA KUA NI KOME KUENDELEA KUMSUMBUA MSICHANA WAKE,NILIJIKUTA MACHOZI YAKINITOKA KWA UCHUNGU NIKIFKILIA MWENENDO WA MAHUSIANO YANGU YALIYOPITA NA HIKI NINACHOKIPITIA.

Nilikata kabisamawasiliano na huyo binti ila alikuja kunitumia meseji akisema kua nimsamehe kwni kitendo kile hakufanya kwa makusudi ingawa ni kweli yuko ndani ya mahusiano mapya hivyo nimuwie radhi..iliniuma sana NIKIKUMBUKA NILIVYOMPENDA KWA MOYO WOTE NIKAMPA KILA 7BABU YA KUNIPENDA KILA SIKU KIASI WATU WALIOKUA WAKITUONA WALITAMANI WAWE SISI ,NA PIA MAMBO MENGI YA KUSISIMUA NILIYOSHIRIKIANA BUT KAMA MSHUMAA UNAVYOWAKA MPAKA KUZIMA,NDIVYO ILIVYOKUA,KWA MAUMIVU MAKARI SANA ,NIKAACHANA NA YULE (COZ WAT GOES AROUND COMES BACK AROUND DADA YULE AKIWA KWAO UGANDA ALIKUJA NIKUMBUKA NA KUNISUMBUA KILA SIKU,LAKIN KWA KILE ALIKFANYA SIKUTAMANI KABISA KURUDI MAANA NGOZI YA CHUI SIKU ZOTE HAIBADIRIK SO ANGEKUJA KURUDIA TENA niliamua niachane kabisa na mapenzi richa ya wasicha na kazaa kutaka ukaribu na mimi,lakini sikua na hamu nao tena mana kikubwa ilikua ni kulinda heshima yangu,sikupenda nilivoonekana kwa watu kua nabadili wanawake..hivo nilikaa mda mlefu bila kua na mahusiano ya kimapenz na mwanamke yeyote na sasa nikiwa nimeajiriwa kwenye kampun flan hapa mwanza bado kama hitaj la binadam yeyote anaejtambua..nahitaj niwe na mwenzangu..mwanamke tutakaeanzisha mahusiano yenye furaha na upendo...

CWEZ KUWACHUKIA WANAWAKE WOTE SABABU NAJUA C WOTE..NAJUA KUNA BINT SEHEM MWENYE HITAJ KAMA LANGU...LAKIN HAJAWAI PATA NAFAS NA MWANAMUME ANAEMSTAHILI HIVO KUPITIA PAGE HII..NAAMIN KUNA WATU WAZIMA.GREAT THINKERS NA WANAOJITAMBUA NINGEPENDA NIPATE MAWZO NA HTA USHAURI AMBAO UTANJENGA LAKIN PIA KMA YUPO BINT MWENYE MAPENZ YA KWELI ANAEJITAMBUA BAS ANITAFUTE FOR HAPPY N LONG LASTIN RELATIONSHIP CFA:mapenz ya kweli.
rangi yoyote. mvumilivu/mwenye heshima. mcha mungu. ili tusipishane sana kimawazo ni vizuri akiwa na elimu kuanzia kidato cha nne na kuendelea. namba yangu ni:0786696226 NI VIZURI UKINITEXT NAMI NITAKUTAFUTA..AHSANTENI
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ushauri wangu kaka muombe mungu sana kwa uwezo wake iko siku utampata wakweli,subra muhimu maishani

    ReplyDelete
  2. Cku hz bhana 99% ya madem ni vcheche wanarelation zaidi ya moja so take care wanauza haoooo...!!!!

    ReplyDelete
  3. omba kwa mungu utapata aliye sahihi kwako. wala usikate tamaa halafu hawa unawita warembo si wazuri sana kwa ssb wanawwke warembo wapo kwa ajili ya kustarehesha wanaume. so watakusumbua sana.

    ReplyDelete
  4. Yan masichan ya siku hizi mangese kweli amepata mtu anayempenda kweli badala ya kutulia anaanza kurukaruka ndio wanaume wengi siku hizi wanawashit wanawagonga na kutupa kule sheenz type...!

    ReplyDelete

Top Post Ad