Volkano Yalipuka Kisiwani..Mmoja Afariki na Wengine 27 Hawajulikani Walipo Mpaka sasa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

New Zealand
Watu 23 wameokolewa huku Polisi ikitahadharisha uwezekano wa kuongezeka kwa vifo katika tukio hilo lililotokea muda mfupi baada ya Watalii kuonekana karibu na mlima huo

Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Jacinda Ardern amesema oparesheni za kuwatafuta manusura zimeanza lakini moshi mkali katika eneo hilo unazuia juhudi hizo

Mlima uliolipuka volkano upo katika Kisiwa kijulikanacho kama 'White Island' maarufu "Whakaari" ikiwa ni moja ya maeneo yenye milima mingi yenye volkano

Licha ya hivyo, Kisiwa hicho huwavutia Watalii ambao huzuru mara kwa mara nyakati za mchana kutokana na kuwepo kwa ndege zinazoendesha shughuli za kitalii

Desemba 3, 2019 Wanajiolojia walitahadharisha kuwa mlima huo huenda ukalipuka kupita kawaida yake, japo waliongeza kuwa kiwango hicho cha mlipuko hakiwezi kuhatarisha maisha ya Watalii
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad