Kauli Kangi Lugola Baada ya Rais Magufuli Kumtumbua na Kusema Hafai

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema ataendelea kumsaidia Rais  Magufuli   kwa kuwa yeye ni mbunge wa Mwibara (CCM).

Lugola ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Januari 23, 2020  jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kumalizika hafla ya uzinduzi wa nyumba za  maofisa wa Jeshi la Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.

Alieleza hayo baada ya Rais  Magufuli  ambaye wakati akizungumza  katika uzinduzi huo kusema Lugola na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias  Andengenye hawafai kuendelea na nyadhifa zao kutokana na mambo waliyoyafanya kuhusu uingiaji wa mikataba.

“Rais ndiye aliniteua kwenye Baraza la Mawaziri na ndiye ameona anipumzishe, kwangu mimi ni jambo la faraja, Watanzania mmemsikia Rais hatua aliyochukua ni hatua nzuri na inalenga kujenga safu ya Serikali, ninaahidi kama Mbunge ambaye nilipata nafasi ya kumsaidia Rais nitaendelea kumsadia kwa kwa heshima kubwa." Amesema Lugola
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad